Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Spika awapa mbinu CHADEMA ili awafukuze akina Mdee

Jumatatu , 3rd Mei , 2021

Spika wa Bunge Job Ndugai, amemuagiza Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) John Mnyika, kuandika barua ambayo ataambatanisha na katiba ya chama chake pamoja na muhtasari wa kikao kilichofanya maamuzi ya kuwafukuza uanachama wabunge 19 wa chama hicho.

kushoto ni Katibu Mkuu wa CHADEMA John Mnyika na kulia ni Spika wa Bunge Job Ndugai

Kauli hiyo ameitoa hii leo Mei 3, 2021, Bungeni Dodoma, hii ni baada ya uwepo wa malalamiko kutoka kwa viongozi wa chama hicho wakimtuhumu Spika Ndugai kutozingatia katiba kwa kuendelea kukaa Bungeni na wabunge wasiokuwa na sifa za ubunge.

"Aandike barua aambatanishe na katiba ya chama chake, aniambatanishie na muhtasari wa hicho kikao kilichofanya hayo maamuzi, inawezekana huyo Katibu Mkuu kaamka tu kaandika halafu na mimi nakurupuka nachukua hatua, nitakua ni Spika au kitu cha ajabu, hivyo andika ili ile barua niwape watalam waangalie, halafu namuuliza msajili wa vyama hawa wajumbe walioorodheshwa ndiyo wajumbe halisi?", amesema Spika Ndugai

"Pia naangalia kwenye muhtasari ule je hawa wabunge wanaotuhumiwa kufukuzwa walipata nafasi hata ya kujieleza na walisikilizwa?, nifukuze watu ambao hawakusikilizwa popote, yaani mbunge hujawahi kusikilizwa wanaandika tu fukuza hawa, viko vyama vimejaa mfumo dume, kundi la wanaume wamekaa wanafukuza wanawake 19 kwa mpigo hata kama barua hiyo inatoka CCM lazima nitawaambia 'stop' kwanza taratibu", ameongeza Spika Ndugai.

Novemba 25, 2020, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kiliwafukuza uanachama wabunge wake 19, akiwemo Halima Mdee, Ester Bulaya, Esther Matiko, Tunza Malapo, Salome Makamba na wengineo kwa madai ya kwamba ni wasaliti baada ya kwenda kula kiapo Bungeni cha kuwa wabunge wa viti maalum kinyume na makubaliano ya chama chao.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava