Jumatano , 17th Mei , 2023

Takwimu za Afya zinaonyesha ugonjwa wa shinikizo la juu la damu ndio unaongoza miongoni mwa magonjwa yasiyoambukiza nchini Tanzania ambapo wagonjwa waliongezeka kutoka 688,901 kwa mwaka 2017, hadi kufikia wagonjwa 1,345,847 kwa mwaka 2021 sawa na ongezeko la asilimia 95.4% 

Takwimu hizo zimetolewa leo Jijini Dodoma na Waziri wa Afya Ummy Mwalimu wakati akitoa tamko la siku ya shinikizo la juu la Damu Duniani ambalo hufanyika kila tarehe 17.05 nakusema nisawa na kila wagonjwa 10 wanaoonwa na wataalamu wa Afya ni wagonjwa 6 wana ugonjwa wa Shinikizo la juu la damu.

Katika kipindi hicho ambacho takwimu hizo zinaonyesha  wagonjwa wenye shinikizo la damu wameongezeka takribani mara mbili zaidi kwa kipindi cha miaka mitano kwa mujibu wa ripoti ya  Health Statistical Bulletin 2022