
Waziri wa Katiba na Sheria Dkt Damasi Ndumbaro
Amesema Katiba iliandikwa tangu mwaka 1977 na kwa sasa kuna mazingira tofauti yanayokinzana na Katiba hiyo
Waziri Ndumbaro amesema kumekuwepo na falsafa nyingi kuhusu Katiba hivyo katika kipindi cha mwaka huu watalaam watafanya tathmini kwa kuwa katika mjadala wa Katiba mpya unaoendelea kwa sasa wengi wanaoongea ni wanasiasa na kusahau kwamba wananchi nao wana nafasi yao ya kutoa maoni yao baada ya kuelewa mazuri na mabaya yaliyomo kwenye Katiba
Katika hatua nyingine waziri Ndumbaro ameeleza kuwa serikali inakwenda kujenga taasisi jumuishi za Sheria tofauti na ilivyo kwa sasa na kwa kuanzia wanakwenda kujenga kwenye majiji na kwenye manispaa
Amesema sababu za kufanya hivyo ni kuondoa usumbufu kwa wananchi wanapotaka kupata huduma katika taasisi hizo za kisheria kufanya kazi maeneo tofauti na pale mwananchi anapohitaji Huduma kulazimika kutumia gharama kubwa kuzifikia huduma hizo