Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Rais Samia aongoze hadi 2030 - Nape Nnauye

Jumamosi , 3rd Dec , 2022

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari na mbunge wa Mtama Nape Nnauye amesema yeye ni miongoni mwa watu wanaopiga debe Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kuchaguliwa katika uchaguzi wa 2025 hadi 2030 ili amalizie kazi ambayo ameianza

Nape ametoa kauli hiyo katika mjadala uliofanyika kwa njia ya mtandao (Zoom) ukiwakutanisha wadau mbalimbali kuhusu maendeleo ya mikoa ya kusini 

"Mimi ni katika wale wanaopiga debe wazi kabisa bila aibu, kwamba mama anastahili kuongezewa muda, akimaliza 2025 tumchague tena hadi 2030, tuna hakika akifika huko atakuwa ametufanyia kazi nzuri kwa mujibu wa katiba yetu atakuwa ndio wakati wa kupumzika" 

Aidha Nape amesema Rais Samia ameacha alama na amerudisha matumaini kwa watu waliokuwa wamepoteza matumaini 

"Rais Samia amerudisha matumaini mahali ambapo watu walianza kukata tamaa, amerudisha furaha mahali ambapo watu walianza kuvunjika moyo, amerudisha upendo mahali ambapo kulikuwa na chuki pengine, na ametuleta pamoja kama watanzania, jambo hili ni kubwa sana"

Kuhusu mikoa ya Lindi na Mtwara na maendeleo yake Nape amesema mikoa hiyo imeanza kupiga hatua kmaendeleo tofauti na watu wanavyoifikiria

"Mikoa ya Lindi na Mtwara ni mikoa ambayo kwa muda fulani hivi ilikuwa nyuma kimaendeleo na ni kwa sababu za kihistoria"

"Mimi jimbo langu la Mtama kwa miaka mitano tulikuwa tunapata fedha kidogo sana za ujenzi wa barabara, baada ya kuanzishwa kwa TARURA haikutengewa fedha ila Rais Samia alivyokuja akatenga fedha bungeni zikaja milioni 500 kwa majimbo yote"

Aidha mbunge wa Lindi Hamida Abdallah amesema serikali ya awamu ya sita imekuwa na kasi kubwa ya maendeleo ikiwemo upatikanaji wa maji safi na salama 

"Kwa kipindi hiki cha awamu ya sita tumeona kasi ya maendeleo inakuja kwa kasi kubwa sana, Lindi kulikuwa na changamoto kubwa sana ya upatikanaji wa maji safi na salama lakini serikali imeweka nguvu wametuoatia fedha zaidi ya bilioni 9" 

"Eneo ambalo limesahaulika ni Lindi mjini lakini ukiangalia namna ambavyo mji ulikuwa na sasa hivi ulivyo kumekuwa na mabadiliko makubwa, kumekuwa na barabara za lami, taa za barabarani na serikali imetuhakikishia fedha kwa ajili ya miradi ya kimkakati"

Kuhusu uwekezaji katika gesi Mkurugenzi Mkuu TPDC James Mataragio amesema ujio wa mradi wa LNG utaongeza pato la taifa na kukuza uchumi wa watanzania huku akiweka wazi kuwa tayari wananchi hususani mikoa ya kusini wameanza kuona matunda ya gesi 

"Mradi wa gesi wa LNG tunategemea utaleta mtaji wa kiasi cha dola za kimarekani bilioni 40, ni fedha nyingi sana na hivi karibuni mradi huu umekuwa namba moja kwa nchi hizi za kusini mwa Afrika" 

"Tayari nchi inafaidi uchumi wa gesi, mpaka leo tunapoongea asilimia 70 ya umeme wote unatumia gesi asilia, kwamba ule umeme unaozalishwa unatumia gesi asilia, ni kwamba tayari wananchi wa mikoa ya kusini wanafaidi matunda ya gesi" 

Mjadala huo pia umehudhuriwa na Mrajisi wa vyama vya ushirika na mtendaji Mkuu tume ya maendeleo ya ushirika Dkt Benson Ndiege na Mkurugenzi wa bodi ya Korosho Francis Alfred, 

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava