Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Nyumba aliyoishi Mwalimu Nyerere yazinduliwa

Jumamosi , 17th Oct , 2020

Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangalla amesema katika wizara hiyo wameanzisha mkakati maalum wa kumuenzi Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na tayari wameunda kamati maalum ambayo itashughulika na suala hilo.

Nyumba ya Hayati Baba wa Taifa Mwl. Julius Nyerere, iliyoko maeneo ya Magomeni

Dkt Kigwangalla amesema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa nyumba kumbukizi ya Mwalimu Julius Kambarege Nyerere aliyowahi kuishi wakati wa harakati za kudai uhuru iliyopo Magomeni jijini Dar es salaam 

“Tayari nimeshaunda kamati itakayosimamia kuhakikisha yale mambo ambayo Baba wa Taifa ameyafanya yanaenziwa, sambamba na kuviweka vitu vyote alivyotumia kama kumbukumbu muhimu kwa taifa.’’amesema Dkt.Kigwangalla. 

Kwa upande wake Waziri Mkuu Mstaafu Jaji Joseph Sinde Warioba amesema Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere bado hajaenziwa ipasavyo, hivyo kumtaka Waziri Kigwangalla kushirikiana na Mkurugenzi wa Makumbusho ya Taifa kufanya maboresho yote ya maeneo ambayo Baba wa Taifa alikua akifanya kazi.

“Bado kuna maeneo mengine ambayo Baba wa Taifa ameyatumia wakati wa harakati za kudai uhuru,hiyvo yanapaswa kutambulika kihistoria’’, amesema Jaji Warioba

Naye mtoto wa Hayati Baba wa Taifa ,Mwalimu Nyerere,Makongoro Nyerere, akiwa mmoja wa waliohudhuria uzinduzi wa nyumba kumbukizi, amefurahishwa na jinsi serikali inavyomuenzi baba yao na kuwasihi Watanzania kujifunza historia aliyoiacha Baba wa Taifa na si kusubiri siku maalum

Nyumba hiyo imezinduliwa leo baada ya ukarabati, ilitumiwa na Baba wa Taifa wakati wa harakati za kudai uhuru na ndani yake vimehifadhiwa vitu mbalimbali alivyotumia Mwalimu ikiwemo cherehani iliyotumika kuzishona nguo zake. 

 

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava