Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

"Nilishasema damu ya Mtanzania haiendi hovyo"- IGP

Jumanne , 15th Sep , 2020

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Simon Sirro, amesema kuwa licha ya kwamba chanzo cha moto ulioteketeza bweni la Shule ya Byamungu Islamic hakijajulikana, lakini bado wanatafuta vyanzo vingine na kudai kuwa huenda kuna adui mwingine aliyesababisha maafa hayo.

Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro

IGP Sirro ametoa kauli hiyo alipofika kwenye eneo la tukio la moto ulioteketeza bweni la shule hiyo, na kuongeza kuwa hata mifumo ya umeme katika jengo hilo haikuwa mizuri pamoja na jengo lenyewe halikuwa madhubuti na kwamba uchunguzi bado unaendelea.

"Jengo lenyewe sijui hata Afisa Elimu na wakaguzi walikuwa wanajua watoto wanalala kwenye hili jengo, tunajaribu kutafuta vyanzo vingine inawezekana jengo halikuwa madhubuti, lakini inaweszekana kuna adaui wa nje amechukua huo mwanya kufanya uhalifu", amesema IGP Sirro.

"Tutafanya upelelezi wa kina na tutapata majibu, niwahakikishie tukipata taarifa sahihi tutawashughulikia kweli kweli, hatuna mchezo na mtu ambaye kwa uzembe wake au nia yake ovu anasababisha vifo, niliwahi kusema damu ya Mtanzania huwa haiendi hovyo, akishakufa Mtanzania lazima aliyesababisha tumshughulikie kwa mujibu wa taratibu", ameongeza IGP Sirro.

Tukio la ajali ya moto katika shule ya Byamungu Islamic iliyoko wilayani Kyerwa mkoani Kagera, lilitokea usiku wa kuamkia jana Septemba 14, 2020, na kupelekea vifo vya watoto 10 na wengine 7 kujeruhiwa, ambapo bweni hilo lilikuwa na wanafunzi 74.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava