Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Miguna apigwa chini, Sonko afanya maamuzi

Jumatano , 13th Jun , 2018

Gavana wa Mji Mkuu wa Kenya, Nairobi Mike Mbuvi Sonko amesema atachagua mgombea mwingine nafasi ya Naibu Gavana wa Nairobi baada ya bunge la kaunti ya Nairobi, Jumanne hii kukataa uteuzi wake wa Mwanasheria Miguna Miguna.

Katika taarifa kwa vyombo vya habari, Sonko amesema atatoa jina jingine baada ya "ushauri wa kutosha."

"Nitawasilisha mteule mwingine aliyestahili kwenye bunge la kaunti ya Nairobi baada ya kushauriana kwa kuhakikisha kuwa Nairobi inapata Naibu  Gavana anayestahili kusaidia katika utoaji wa huduma," amesema Sonko.

Aidha ameeleza kwamba "Ninataka kukubali uamuzi wa bunge la kaunti ya Nairobi kukataa uteuzi wa Dk Miguna Miguna kama Naibu Gavana wa Nairobi kwa sababu ya uraia kama ilivyoelezwa kwenye  kifungu cha 78 cha Katiba."

Mbali na hayo Spika wa bunge Beatrice Elachi,  Jumanne hii  alielezea kwamba hakuwa na uwezo wa kujadili uteuzi wa Miguna kwa sababu afisa wa Serikali hawezi kushikilia uraia miwili.

Hata hivyo Serikali ya Kenya  imesisitiza mara kwa mara kwamba Miguna si raia wa Kenya, kwa hivyo, ataruhusiwa tu kuingia nchini humo kwa kutumia pasipoti yake ya halali ya Canada.

Katibu Mkuu wa Uhamiaji Gordon Kihalangwa alisema Miguna lazima aomba tena upya kurejesha uraia wake nchini Kenya.

Mei 17 mwaka huu Gavana Sonko alimpendekeza Mwanasheria Miguna kuwa Naibu Gavana wa Mji wa Nairobi.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava