Alhamisi , 22nd Aug , 2024

Seleman Kibiki (46) aliyekuwa ni fundi wa magari na mkazi wa Kiluvya, Kisarawe mkoani Pwani, alijinyonga Agosti 13 akiwa kwenye mahabusu ya mahakama akisubiri kupelekwa gerezani baada ya kutiwa hatiani na Mahakama ya wilaya ya Kisarawe kwa kosa la kumbaka na kumlawiti mtoto wake wa kufikia

Kamanda wa Polisi mkoa wa Pwani

mwenye umri wa miaka 7 siku ya Februari 13 mwaka huu.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Polisi mkoa wa Pwani, Kibiki alichukua uamuzi huo mara baada ya kusomewa hukumu hiyo na aliamua kuingia chooni kisha kujinyonga kwa kutumia shati lake ambalo alilifunga kwenye nondo za dirisha la choo hicho.

Aidha katika hatua nyingine, katika kipindi cha mwezi Julai 2024 mpaka sasa jumla ya washtakiwa saba wamehukumiwa vifungo vya miaka 30 jela na wengine wakifungwa maisha kwa makosa ya kubaka, kulawiti na kuzini na maharimu wao.