Jumatatu , 9th Mar , 2026

Mchezaji raia wa Uruguay Sebastián Abreu maarufu kama "El Loco" anashikilia rekodi ya dunia ya kuwa mchezaji aliyebadilisha Klabu nyingi zaidi duniani.

Sebastián Abreu maarufu kama "El Loco"

"El Loco" Alichezea zaidi ya vilabu 32 tofauti katika nchi tofauti tofauti kuanzia mwaka 1994-2021, akifanikiwa kufunga magoli zaidi ya 400 katika michezo zaidi ya 800 aliyocheza.

Miongoni mwa klabu alizocheza ni pamoja na River Plate (Argentina), Real Sociedad (Spain), Botafogo (Brazil), Club America (Mexico) na Beitar Jerusalem (Israel)