Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Maua Sama awaibua BoT, watoa tamko

Jumatano , 19th Sep , 2018

Benki kuu ya Tanzania (BOT) imetoa onyo kwa wananchi kuheshimu fedha ya Tanzania kwakuwa ni moja ya alama ya taifa na kuonya kwamba kudhihaki na kukejeli noti na sarafu ni kosa la jinai.

Msanii wa muziki wa bongo fleva Maua Sama.

Tamko hilo limetolewa kufuatia matukio ya hivi karibuni ya baadhi ya wananchi kuonekana wakifanya dhihaka noti za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuzirusha ovyo na kuzikanyaga. Hali iliyopelekea wengine kuchukuliwa hatua za kukamatwa na Jeshi la Polisi akiwemo msanii wa muziki wa kizazi kipya Maua Sama baada ya kuweka 'video' kwenye mtandao wake wa kijamii ikionyesha wakichezea noti ya shilingi elfu kumi huku wakiimba wimbo wake mpya unaokwenda kwa jina la 'Iokote'.

Taarifa ya BoT kwa vyombo vya habari ambayo wameitoa, inasema utunzaji mzuri wa fedha utapunguza uwezekano wa fedha hizo kuchakaa mapema na kupunguza gharama za uchapishaji.

"Kwa mujibu wa Sheria ya Benki Kuu ya Tanzania ya mwaka 2006, kifungu cha 26, BoT ndiyo taasisi pekee yenye mamlaka ya kutoa noti na sarafu katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania," imesema taarifa hiyo.

Taarifa imesisitiza kuwa, “Benki Kuu pekee ndiyo yenye mamlaka ya kuharibu noti na sarafu (kifungu cha 28 kikisomwa pamoja na kifungu cha 30 cha Sheria ya Benki Kuu ya Tanzania ya mwaka 2006”.

Msanii Maua Sama ambaye taarifa ya kukamatwa kwake ilitolewa Kamanda wa Polisi mkoa wa Dar es salaam, Lazaro Mambosasa hadi sasa bado anashikiliwa polisi katika kituo cha kati jijini Dar es salaam toka siku ya Jumapili na hadi sasa taarifa zinasema bado hawajafikishwa mahakamani uchunguzi zaidi ukiendelea.

Soma zaidi hapo chini taarifa ya BoT.

 

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava