Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mapacha walioungana waaga dunia

Alhamisi , 17th Aug , 2017

Mapacha walioungana kuanzia kifuani hadi tumboni wamefariki dunia jana katika hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam walipokuwa wakipatiwa matibabu baada ya kuzaliwa katika hospitali ya Berege wilayani Kilosa mkoani Morogoro.

Afisa uhusiano wa hospitali ya Taifa Muhimbili, Neema Mwangomo amethibitisha kufariki kwa watoto hao ambao walikuwa wakisubiri kufanyiwa upasuaji, huku akisema kuwa uchunguzi unafanyika kubaini chanzo cha kifo cha watoto hao.

Watoto hao waliozaliwa wakiwa na uzito wa kilo nne walipewa rufaa ya kupelekwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili ili kupatiwa uangalizi zaidi na waliwasili katika hospitali hiyo Juni 24 na kuwekwa katika chumba cha uangalizi maalum.

Daktari bingwa wa upasuaji wa watoto, Dkt. Zaituni Buhari Agosti 2 mwaka huu alieleza wanahabari kuwa  watoto hao walikuwa wanachangia ini na sehemu ndogo ya moyo lakini wangeweza kufanyiwa upasuaji.

Hata hivyo baadhi ya mapacha wa aina hiyo ambao hawajawahi kufanyiwa upasuaji na kufanikiwa kuishi na kuwa watu wazima ni pamoja wale wanaoishi wilayani Kilolo mkoani Iringa na wamehitimu kidato cha sita mwaka huu na kupata ufaulu mzuri wa kuendelea na elimu ya juu..

 

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava