Jumapili , 26th Oct , 2025

Makarani hao wameaswa kutokuwa chanzo cha migogoro wakati wa upigaji kura badala yake wafuate miongozo, sheria, kauni na katiba ya tume ya uchaguzi.

Jumla ya Makarani waongozaji 422 wa usimimizi wa Uchaguzi Mkuu katika majimbo mawili ya Bunda na Jimbo la Mwibara wameapishwa.

‎Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo msimamizi  wa Uchaguzi katika Jimbo la uchaguzi la Bunda na Mwibara Oscar Nchemwa amesema makarani hao wanapaswa kusoma na kufuata kanuni na Sheria za uchaguzi ili kuepuka migongano ya kisiasa wakati wa upigaji kura na  kuzua taharuki zisizo na lazima na kuharibu mchakato wa Uchaguzi.