
Wakiongea na East Africa Radio, wakazi hao wamesema ni jukumu la serikali kutengeneza miundombinu hiyo mapema ili kuwanusuru na hali ya wasiwasi waliyonayo ya kuugua ugonjwa hatari wa Dengue.
Kauli ya wakazi hao imekuja wakati ambapo takwimu za wizara ya afya zinaonyesha kuwa zaidi ya watu mia moja wameugua na kulazwa kutokana na ugonjwa huo huku wawili kati yao wakiripotiwa kufariki dunia.