Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Kesi ya wafugaji Ngorongoro yatupiliwa mbali

Ijumaa , 30th Sep , 2022

Mahakama ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, imetupilia mbali maombi ya wananchi wa jamii ya wafugaji ya Maasai katika kesi iliyohusisha mgogoro wa ardhi baina ya serikali ya Tanzania na wananchi hao wa wilaya ya Ngorongoro mkoani Arusha, baada ya wafugaji hao kushindwa kuthibitisha madai yao.

Wafugaji wa Kimaasai

Mahakama ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, imetupilia mbali maombi ya wananchi wa jamii ya wafugaji ya Maasai katika kesi iliyohusisha mgogoro wa ardhi baina ya serikali ya Tanzania na wananchi hao wa Ngorongoro mkoani Arusha, baada ya kushindwa kuthibitisha madai yao.

Akisoma maamuzi hayo ya mahakama JajI Charles Nyachae kwa niaba ya Jaji Monica Mugenyi, amesema kuwa waleta maombi ambao ni wafugaji wa jamii ya kimaasai walishindwa kuthibitisha madai yao ya kwamba waliteswa na kupigwa pamoja na kuharibiwa mali zao na watu waliowataja kuwa ni askari wa jeshi la polisi la Tanzania wakati wakiwaondoa kwenye makazi yao. 

Katika utetezi wao Mwanasheria Mkuu wa serikali ya Tanzania amebainisha kwamba, waliwaondoa wafugaji waliovamia Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, ambayo inapakana na eneo la Ngorongoro upande wa Kaskazini, na sio kweli kwamba waliwaondoa katika maeneo ya vijiji vyao kwa nguvu na kwa kuwatesa. 

Maelezo ya waleta maombi yaliyosomwa mahakamani hapo yanasema  kuwa miongoni mwa mashahidi walieleza jinsi walivyoshuhudia wananchi wakipigwa na watu wanaoaminika kuwa maafisa wa jeshi la polisi la Tanzania, na walishuhudia magari yaliyobeba askari wa polisi na pia waliwashuhudia maafisa wakiharibu nyumba, mifugo na mali zingine za wakazi hao. 

Baadhi ya Mawakili wa upande wa wapeleka mashtaka  na wakazi wa Ngorongoro wamesema hawajaridhika na maamuzi hayo na kwamba watakata rufaa.

Maelezo ya upande wa  serikali katika utetezi wa tuhuma hizo, yanabainisha kwamba serikali ina haki ya kuichukua ardhi hiyo na kwamba haikutumia nguvu wala uvunjifu wowote wa haki za binadamu wakati wa kuendesha zoezi hilo.  

 
 

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava