Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Kesi kupinga sheria mpya ya habari yafunguliwa

Jumatano , 11th Jan , 2017

Baraza la Habari Tanzania, Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) wamefungua kesi kupinga baadhi ya vipengele vya Sheria ya Huduma za Vyombo Vya Habari ya 2016.

Kajubi Mukajanga - Katibu Mtendaji wa MCT

Kesi hiyo imefunguliwa katika Mahakama ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EACJ), ambayo ofisi zake ziko katika jengo la Mahakama ya Rufani, jijini Dar es Salaam chini ya mawakili Fulgence Massawe, Donald Deya, Jenerali Ulimwengu, Jebra Kambole, Francis Stolla na Mpale Mpoki ambao wanaziwakilisha taasisi hizo.

Katika kesi hiyo, washirika hao wanataka baadhi ya vifungu kwenye sheria hiyo ambavyo vinakandamiza uhuru wa habari na uhuru wa kujieleza vifutwe kwa madai kuwa vinakiuka matakwa ya mkataba wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ibara za 6(d) na 7(2).

Akitoa taarifa hiyo kwa waandishi wa habari, Katibu Mtendaji wa Baraza la Habari Tanzania (MCT) Kajubi Mkajanga amesema kwa mujibu wa kifungu cha 8 (1) c , Tanzania inapaswa kuchukua hatua kuhakikisha haki zote zinazotajwa katika mkataba huo zinafuatwa na kutekelezwa.

Amesema Tanzania iliridhia mkataba huo Julai 7, 2000 chini ya kifungu namba 23 cha mkataba huo, mahakama imepewa mamlaka ya kutafsiri mkataba huo na kuhakikisha nchi wanachama wanaufuata na kuusimamia.

Sheria hiyo ilipitishwa na Bunge Novemba 5 mwaka jana na baadaye kuidhinishwa na Rais Magufuli Novemba 16 mwaka jana.

Wasikilize hapa, Kajubi (MCT), Bi Helleni Kijo Bisimba (LHRC) na Onesmo Olengurumwa (THRDC)

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava