Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Kamanda aliyewaonya wanaume azungumzia kuhamishwa

Jumanne , 22nd Mei , 2018

Aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mjini Magharibi Visiwani Zanzibar, Hassan Nassir Ali, amefunguka juu ya uhamisho wake aliopewa siku chache baada ya kuwaonya wanaume juu ya tabia zao zisizofaa kwenye jamii.

Akizungumza na www.eatv.tv, Kamanda Hassan amesema kwamba uhamisho wake ni wa kawaida na wala haujatokana na kauli alizotoa, ambazo zilizua gumzo kwenye mitandao ya kijamii.

Akiendelea kutolea ufafanuzi suala hilo Kamanda Hassan amesema kwamba kauli hiyo aliitoa na alikuwa anamaanisha, lakini haijaleta mtafaruku wowote kwenye jamii kama ambavyo inasemekana, na hata walipoijadili kwenye Baraza la Wawakilishi Zanzibar ilikuwa ni utani.

“IGP amesema mwenyewe amefanya uhamisho na uteuzi huu ili kuimarisha safu yake kiutendaji, mimi ningekuwa nimesema nimewakwaza watu sio kweli, hata wale waliosema katika Baraza la Uwakilishi ilikuwa ni kwa utani, ni uhamisho wa kawaida kabisa, wala sio chuki”, amesema Kamanda Hassan.

Kamanda Hassan ameendelea kwa kuwataka wananchi wa Kaskazini Pemba ambako amehamishiwa kufuata sheria bila shuruti kwani kazi iko pale pale.

“Nitaendelea kufanya kazi yangu vizuri nitaendelea kusimamia sheria vizuri, kazi iko pale pale bado mimi ni Kamanda wa polisi nitasimamia sheria za nchi, wala sio jambo langu hili wala mie sio mzee wa vikohozi, mimi nimetoa mifano, hivyo kazi iko pale pale”, amesema Kamanda Hassan.

Kamanda huyo ambaye metokea visiwani Zanzibar wiki iliyopita aliibua mzozo kwenye mitandao baada ya kuwaonya wanaume wenye tabia ya kukohoa pindi waonapo wanawake wenye maumbile makubwa, akisema hilo ni kosa kisheria ambalo linatambulika kama shambulio la aibu.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava