
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila ameyasema hayo wakati wa kikao cha kujadili maendeleo ya Mkoa ambacho kiliwahusisha viongozi wa dini na taasisi mbalimbali, ambapo amesema tayari wataalam wa Halmashauri ya Jiji la Mbeya wameandaa andiko la kuwasilisha kwenye vikao vyake vya madiwani mara baada ya kuapishwa.
Chalamila amesema mchakato huo ni ahadi aliyoitoa Rais Mteule Dk. John Magufuli wakati wa kampeni za kuomba urais mkoani humo ambapo alidai akipata ridhaa ya kiti hicho ataongeza manispaa ili kusongeza huduma za kijamii karibu na wananchi.
Hata hivyo Mwakilishi wa wabunge wateule wa Mkoa wa Mbeya, Anthon Mwantona kutoka Jimbo la Rungwe, amewahidi wanambeya kuwa kazi kubwa watakayoifanya wabunge hao ni kusimamia na kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo ambayo yatachangia mkoa wa Mbeya kuwa wa mfano bila kujali itikadi za kisiasa.