
Mwili wa David Kahela
Taarifa za kifo hicho zimethibitishwa na Mwenyekiti wa Mtaa huo, Silasi Kayange pamoja na ndugu wa marehemu, Godfrey Kahela ambaye ni kaka wa marehemu.
Kwa sasa chanzo halisi cha kifo hicho bado hakijajulikana, na Jeshi la Polisi limechukua mwili wa marehemu kwa ajili ya uchunguzi wa kina ili kubaini sababu kamili zilizopelekea kifo hicho.
Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi wake na limewataka wananchi kuwa watulivu huku likifuatilia kwa ukaribu tukio hilo la kusikitisha.