Bwawa la mtera limekuwa tegemeo kwa wakazi wa halmashauri za wilaya ya iringa, chamwino na Mpwapwa kwa ajili ya kufanya shughuli za uvuvi na kuendesha miasha yao lakini changamoto kubwa kwasasa bwawa hilo maji yake yanazidi kupungua na samaki kutoweka kutokana na wananchi wanaozunguka bwawa hilo kufanya shughuli za kilimo pembezoni mwa bwawa hilo
Lakini katika kunusuru bwawa hilo Tume ya taifa ya mipango ya matumizi ya ardhi kwakushirikiana na ofisi ya makamu wa rais Mazingira imeanza utekelezaji wa mradi wa uhifadhi wa vyanzo vya maji kwenye vijiji vya makuka ,makatapola na mnadani wilayani iringa ambavyo vinavyozunguka bwawa hilo
Lakini wananchi wanapokeaje mpango huo wa urasimishaji wa ardhi unaoratibiwa na tume ya taifa ya mipango ya matumizi ya ardhi?