watu wawili.
Mtu huyo aliyeuawa kwa kukatwa na kitu chenye ncha kali ni mkazi wa kijiji cha Nyambula kata ya Ngogwa, Halmashauri ya mji wa Kahama aliyekuwa amelala ndani na mkewe Shija Mkela Maziku ambaye yeye alijeruhiwa.
"Chanzo cha tukio hilo kinasadikiwa ni imani za kishirikina, kutokana na tukio la kupigwa na radi mwezi wa Februari, 2019 ambapo ilisababisha kifo cha mdogo wake na marehemu aitwaye Mhoja Kadilanha Salehe (45), mkazi wa Nyambula pamoja na mkewe aitwaye Pili Tabu Mabula (36), mkazi wa Nyambula na wakati wengine waliokuwa pamoja nao hawakupata madhara kutokana na radi hiyo", amesema Kamanda Abwao.
Kamanda ameitaja mbinu waliyotumia waharifu hao ni kuvunja mlango na kumvamia akiwa amelala chumbani kwake na mkewe, ambapo mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya Halmashauri Mji wa Kahama.



