Jumanne , 24th Jan , 2023

Mwanaume mmoja anadaiwa kupoteza korodani zake kufuatia kipigo alichopokea kutoka kwa polisi wakati akipiga picha katika maandamano ya kupinga mageuzi ya pensheni nchini Ufaransa 

Kwa mujibu wa wakili wake Lucie Simon, amesema mwanaume  huyo bado yuko hospitalini na korodani zake zililazimika kukatwa kutokana na kipigo kikali na kwamba atawasilisha malalamishi kwa niaba ya mteja wake ambaye ni mhandisi mwenye umri wa miaka 26.

Wizara ya mambo ya ndani nchini humo imesema kuwa takriban Wafaransa 80,000 waliandamana mjini Paris wiki iliyopita kama sehemu ya maandamano ya nchi nzima kupinga mpango wa Rais Emmanuel Macron wa kuongeza umri wa kustaafu kutoka miaka 62 hadi 64