
Lori liliwka moto Ubungo
Taarifa hiyo imetolewa na Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Kinondoni Mrakibu Mwandamizi Elisa Mugisha, amesema pia takribani vibanda 19 vya wafanyabiashara vilivyokuwa vimeshika moto viliokolewa huku pikipiki mbili zikiteketea.
"Moto wa mafuta una taratibu zake kwenye uzimaji, kazi kubwa tuliyoifanya ni kupoza tanki ili kuepusha lisilipuke na tulifanikiwa kazi hiyo,"amesema Kamanda Kamugusha.
Aidha Kamanda ameongeza kuwa "Ajali haina kinga, ajali haimtaarifu mtu ukiona kuna shida ni vyema kupiga simu kwa watu wa uokoaji ili wafike kutoa msaada kuliko kuishia kurekodi video na kusambaza sio utamaduni,".