Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Waondoleeni wavuvi tozo kubwa - Majaliwa

Jumanne , 20th Sep , 2022

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa ameitaka Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuhakikisha inawawezesha wavuvi wadogowadogo kwa kuwapatia elimu ya uvuvi endelevu na kuzitaka halmashauri kuondoa tozo kubwa kwa wavuvi wadogowadogo.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa  amesema hayo katika uzinduzi wa mpango kabambe wa sekta ya uvuvi 2021/2022 – 2036/2037 Jijini Dar es Salaam, na kuwaagiza viongozi wa wizara sekta ya uvuvi, wakuu wa mikoa na wilaya kuwawezesha wavuvi wadogowadogo kwa kuwapa elimu ya uvuvi endelevu pamoja na kuona namna ya kuondoa shuru mbalimbali kwenye halmashauri zinazowarudisha nyuma wavuvi kiuchumi.

“Nitoe maagizo kuhusu swala la shuru mbalimbali za halmashauri, zisiwe kubwa na nyingi kwasababu tumegundua hizi tozo ndizo zinapelekea wavuvi wadogo katika nchi yetu kuikimbia sekta hii na kukwamisha maendeleo ya uchumi. Lengo ni kuhakikisha ndani ya miaka 10 tuweze kuchangia 10% ya pato la taifa badala ya 1.8% ambayo sekta ya uvuvi inavhangia hivi sasa"- Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

 Aidha, Waziri mwenye dhamana ya uvuvi nchini Mhe. Mashimba Ndaki amesema katika mpango huu wa miaka kumi katika sekta ya uvuvi wamejizatiti kuongeza wawekezaji huku M/kiti wa umoja wa wavuvi akiweka wazi changamoto wanazokutana nazo. 

Sekta hii ya uvuvi ambayo inatajwa kuchangia asilimia 1.8 ya pato la taifa imetoa ajira takribani laki mbili kwa wavuvi wadogo na wadau wengine wapatao Milioni 4.5 nchini, huku ikigubikwa na changamoto lukuki licha ya kuchangia katika upatikanaji wa kipato na usalama wa chakula.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava