
Naibu Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara Exaud Kigahe
Hayo yamesemwa leo na Naibu Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara Exaud Kigahe, wakati wa uzinduzi rasmi wa huduma ya mikopo nafuu kutoka benki ya UBA ijulikanayo kama Mkopo Kitonga na kubainisha kuwa sekta ya wajasiriamali wadogo na wakati nchini ina mchango mkubwa wa kutatua changamoto ya ajira nchini.
Naye Mwenyekiti wa Bodi wa benki ya UBA, amesema bidhaa hiyo mpya ya mikopo waliyoizindua leo imejali wateja wake na wajasriamali ambapo itasaidia kupata mikopo nafuu na kukuza mitaji ya biashara zao.