Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Dkt. Biteko ataka maeneo ya madini yaendelezwe

Ijumaa , 22nd Jul , 2022

Waziri wa Madini Dkt. Doto Biteko ametoa agizo kwa wawekezaji katika Sekta ya Madini kuendeleza maeneo yao yenye madini ya kimkakati badala ya kuyaacha bila kuyaendeleza suala linalopelekea wenye nia ya kuwekeza kukosa fursa hiyo

Amesema wapo wawekezaji wanaotaka kuwekeza katika Sekta hiyo maeneo mbalimbali nchini lakini wanashindwa sababu baadhi yao wanakaa na maeneo kwa muda mrefu bila kuyaendeleza.

Hayo yamebainishwa Julai 21, 2022 na Waziri wa Madini Dkt. Doto Biteko katika kijiji cha Mgambazi wilaya ya Uvinza Mkoani Kigoma alipotembelea Kampuni ya Lubalisi Resources Ltd inayofanya utafiti wa madini ya Nikeli.

Amewasisitiza wawekezaji katika Sekta ya Madini wanapaswa kufuata Sheria na Taratibu zilizowekwa katika uwekezaji huo ili kuepuka kufutiwa leseni zao.

Aidha, amewataka wawekezaji hao kuwasilisha taarifa za kipindi cha miezi mitatu ya utekelezaji kazi ya utafiti wa madini iliyofanyika kwa kipindi husika (quarterly report) ambayo husaidia kujua mwenendo au maendeleo ya mradi ya utafiti wa madini.

Amesema lengo la taarifa hizo ni kuiwezesha Serikali kutambua maendeleo ya mradi kwa kipindi husika.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Uvinza Hanafi Msabaha amewataka wawekezaji kuchangia katika huduma mbalimbali za kijamii ili jamii zinufaike na uwepo wa madini. Amesema ushirikishwaji wa wananchi utasaidia kupunguza malalamiko yanayojitokeza mara kwa mara kuhusu wawekezaji.

Naye, Mratibu wa Mradi na Mawasiliano ya Jamii Ashery Lemelo amemuakikishia Dkt. Biteko kusimamia maelekezo yaliyotolewa na Serikali katika mradi huo.

Katika wilaya ya Uvinza tafiti zinaonesha kuwa na madini ya Nikeli. Madini hayo hutumika katika utengenezaji wa bidhaa za magari ya umeme ikiwemo betri na vifaa mbalimbali vya umeme. Aidha, madini ya mkakati yenye uhitaji mkubwa nchini ni pamoja na madini ya Kinywe.
 

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava