Kauli hiyo imetolewa jijini Dar es salaam na meneja uhusiano na mawasiliano wa Airtel Tanzania Jackson Mmbando wakati akitangaza washindi wa promosheni ya upige mwingi na Airtel inayotarajia kudumu kwa kipindi cha miezi mitatu ambapo wateja wanajishindia zawadi mbalimbali ikiwepo pesa taslimu,friji,pikipiki na flat screen..
Mbando amesema kuwa mpaka sasa kampeni hiyo imeshatoa washindi wa fedha taslimu milioni 15 na zawadi zingine zinaendelea kutolewa ambapo mpaka sasa imebakia miezi miwili na siku 15 ,kati ya miezi mitatu ambayo kampeni itaendeshwa ambapo kila mteja au wakala wa airtel anaponunua bando au kufanya muamala wowote kutumia airtel money ataingia kwenye droo ya kushinda zawadi.