Tanzania, Marekani kuandaa mkutano kujadili Ugaidi
Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na serikali ya Marekani wameandaa mkutano unaolenga kujadili uhifadhi wa wanyamapori katika hifadhi zote nchini hususani wakianza na hifadhi ya Selous.
Hayo yameelezwa leo jijini Dar es salaam na Waziri wa Mali asili na Utalii, Mhe Lazaro nyalandu wakati akipokea helikopta iliyotolewa na tajiri wa Marekani Buffet Haward kwa ajili ya kupambana na tatizo la ujangili wa wanyamapori.
Waziri Nyalandu amesema mkutano huo utafanyika Juni 27 mwaka huu, jijini Dar es Salaam ili kuangalia namna ya kukabiliana na uhalifu wa wanyamapori.

