Mshindi wa Miss Tanga 2014 kujulikana leo
Shindano kubwa kabisa la Nice and Lovely Miss Tanga 2014, linatarajiwa kuwa kivutio kikubwa siku ya leo Jijini Tanga pale Mkonge Hotel, katika tukio ambalo litabarikiwa na ugeni mzito kabisa wa Mkuu wa Mkoa, Luteni mstaafu Chiku Gallawa.

