Mizoga ya Tembo 13 waliouawa na kung'olewa meno na majangili katika pori la Akiba la Piti kata ya Ngwara wilayani Chunya mkoani Mbeya
SERIKALI inakusudia kufanya upya sensa ya tembo, kati ya Agosti na Septemba mwaka huu, katika ikolojia ya Ruaha-Rungwa ili kupata idadi kamili ya wanyama hao ambao wanatishia kupotea kutokana na ujangili.