Kili Stars yamaliza makundi CECAFA bila kupoteza
Tanzania Bara imefuzu kwa kishindo Robo Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge kufuatia kumaliza mechi za makundi bila kupoteza mchezo hata mmoja baada ya kushinda miwili na kwenda sare mchezo mmoja kundi A.