Wazee Mtwara wamlilia Magufuli

Chama cha Wastaafu na Wazee (CHAWAMU) mkoani Mtwara kimeitaka serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, kutatua changamoto zinazowakabili wazee ikiwa ni pamoja na kupitisha sera ya Taifa ya Wazee na kuwa sheria.

Akizungumza mkoani humo, katibu wa chama hicho, Wilberd Nandonde, amesema sera hiyo ambayo ilitungwa toka mwaka 2003 bado haijawa sheria na ni muda mrefu umepita jambo ambalo linasababisha changamoto nyingi zinazowakabili kuto fanyiwa kazi.

Pages

Subscribe to East Africa Television RSS