Hatma ya mji mkongwe Zanzibar mikononi mwa UNESCO
Jopo la wataalamu wa mazingira kutoka shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, UNESCO linatarajiwa kuwasili Zanzibar nchini Tanzania mwishoni mwa juma, kufanya majadiliano na mamlaka visiwani humo kuhusu hatma ya mji mkongwe.

