“Vyakula vya harusini vichunguzwe”-Waziri Ummy
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu ametoa agizo kwa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) na Wizara ya Afya, Kitengo cha Afya ya Mazingira, kuangalia ni Mamlaka ipi inajukumu la kutazama vyakula vinavyoliwa kwenye maharusi, ili kulinda afya za walaji.