RPC ataja chanzo mlipuko wa moto Kigamboni
Kamanda wa Polisi Temeke, Amon Kakwale, amesema chanzo cha moto uliotokea usiku wa kuamkia leo katika matanki ya mafuta ya kampuni ya Lake Oil, eneo la Kigamboni, umesababishwa na hitilafu ya mota inayosukuma mafuta kutoka chini na kupandisha juu, iliyopelekea cheche na kuleta mlipuko.

