Mbowe aukwaa tena
Mbunge wa Hai, Freeman Mbowe, amechaguliwa kwa mara nyingine tena kuongoza kiti cha Uenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), baada ya kupata ushindi wa kishindo kwa kupigiwa kura 886 na kumburuza mgombea mwenzake, Cecil Mwambe aliyepata kura 56 pekee.