Aliyejiuzulu Ukatibu Mkuu, ateuliwa kuwa Balozi
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli, amemteua Meja Jenerali Jacob Kingu kuwa Balozi, kabla ya uteuzi Jenerali Kingu alikuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani, mpaka jana Januari 22, 2020 ambapo aliandika barua ya kujiuzulu nafasi hiyo na akakubaliwa.

