Arteta athibitisha Mosquera na Rice kuumia
Kocha wa Arsenal, Mikel Arteta, amethibitisha kuongezeka kwa orodha ya majeruhi ndani ya kikosi chake baada ya Cristhian Mosquera na Declan Rice kuumia katika ushindi wa 2-0 dhidi ya Brentford kwenye mechi ya Ligi Kuu ya England, iliyochezwa Jumatano, Desemba 3 kwenye Uwanja wa Emirates.

