Friday , 22nd Sep , 2023

Kwenye mahojiano yake na kipindi cha Planet Bongo, Msanii wa Bongofleva Rashidi Abdala Makwilo maarufu kama Chid beenz, alifunguka kwa kusema moja kati ya watayarishaji wa muziki ambao alikuwa akifurahishwa sana pindi wanapofanya kazi ni marehemu Pancho Latino.

''Ingawa ma-paroducer wote na-enjoy kufanya nao kazi, lakini lazima ni mtaje pancho na nikitoka kumtaja pancho lazima nimtaje Allen Mapigo, kwa sababu nilifanya nao Dar es salaam stand up, na Pancho kwa sasa ni marehemu kwahiyo ni lazima niwakumbushe kwamba Dar es salaam stand up kafanya Pancho Latino'' alisema Chid Beenz.

Mbali na Chid Beenz kuwa na mpango wa kuja na ''remix'' ya wimbo wa Dar es salaam stand up amefunguka pia kwa kusema bado yupo kwenye kufahamu ni nani awepo, vilevile wapo baadhi ya mashabiki zake wanaomba usifanyiwe ''remix'' ili kutunza ubora wa wimbo huo.