
Wakazi hao wameeleza furaha yao baada ya kuuawa kwa mamba huyo, ambapo wamesema amekuwa akiwaletea athari kubwa ikiwemo kusababisha vifo suala lililowafanya waogope kuchota maji ziwani na kupelekea kukosa huduma za muhimu
Hatua ya TAWIRI kuanzisha oparesheni vuna mamba imekuwa tumaini kwa wakazi wa maeneo hayo kwa kusaidia kuuawa kwa mamba mmoja aliyekuwa kero kubwa kisha kugawiwa kwao kama kitoweo