Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Sept.1 Mfaume, Pialali kurudiana

Thursday , 16th Mar , 2023

Mabondia wawili mahasimu, Iddy Pialali na Mfaume Mfaume leo wamesaini mkataba wa kurudiwa kwa pambano lao linalotarajiwa kufanyika Septemba Mosi, mwaka huu, tukio lililofanyika viwanja vya Leaders Club, Dar es Salaam huku kila mmoja akitamba kumaliza pambano mapema.

Pambano hilo lililopewa jina la King Of The Night linaloteka hisia za wengi kutokana na upinzani uliopo baina yao na kambi zao, linarudiwa baada ya lile la awali lililopigwa Arusha kuvunjika baada ya kutafsiriwa mabondia hao waligongana vichwa vilivyopelekea Pialali kupasuka usoni.

Pambano hilo lililokuwa la raundi 10 lililopigwa Desemba 26, mwaka jana na lilivunjika raundi ya kwanza.

Hata hivyo mara baada ya kuingia mkataba huo, Mfaume alitamba kuwa atahakikisha anamchakaza mpinzani wake na kama haitakuwa hivyo basi ataacha mchezo wa ngumi.

“Tusiangalie yaliyopita ilikuwaje, Watanzania wote waliona kilichotokea, hakuna kichwa ni uoga tu, sasa siku hiyo kukimbia hakuna. Mama Mfaume amesema mwanangu ‘kaza buti’.

“Tangu niko mdogo, mama yangu ananiambia hivyo, maana yake pambana, fanya mazoezi kwa bidii halafu kasema raundi ya tatu mwisho, Bi Mkubwa nimenuukuu kauli yako, huyu asipoamkia ICU (chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalum), naacha boxing.

“Mama Mfaume kaongea na timu yangu timu ya Mabibo siongei sana, nasemaje tupigane mpaka mmoja afe,” alisema Mfaume.

Naye Pialali alisema: “Mapepe, muoga anatetemeka tetemeka, mwanaume anaongea sana? Mwanaume haongei sana. Nasema niko, safi niko salama, Mfaume safari hii kazi anayo, huyu (Mfaume) ni kondoo sio bondia sasa huyu kondoo dawa yake nishaipata tayari, kuna watu anawategemea lakini huyu kondoo nampiga ‘KnockOut’ mbaya sababu sio bondia, hamalizi huyu hana maajabu.

“Mfaume kampiga nani hapa Tanzania? Sisi tunacheza ngumi hatuogopi, kazi anayo, Manzese msiwe na presha, hapa anajikaza tu ila tutampiga,” alisema Pialali.

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea