Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Binti (12) abakwa na kuuliwa Mwanza

Thursday , 16th Mar , 2023

Binti wa miaka 12 amefariki kwa kubakwa na kuchomwa kisu na watu wasiojulikana huko Pasiansi, Manispaa ya Ilemela, Jijini Mwanza.

Inadaiwa wabakaji hao walimvamia usiku anapoishi na bibi yake na kumbaka kisha kumchoma kisu shingoni kitendo kilichompelekea kupoteza  maisha wakati bibi yake akiwa kwenye shughuli zake za kuuza chakula.

Akielezea tukio hilo Bibi wa muathirika wa tukio hilo, Bi Mwanne Hassan amesema alimkuta mjukuu wake akiwa amelala mlango wazi lakini hata alipomuita hakuitika.

 "Nilipomaliza biashara nakurudi ndipo nilikuta mlango wazi, ilikuwa saa saba usiku nikafika nikasema mbona mlango upo wazi? Nikaingia ndani nakumuita lakini hakuitika, nikamshika nikaona amelegea hasemi kitu nikapiga kelele watu wakaja nikawauliza hamkusikia chochote? tulipompeleka pale Sabatho hospitali wakamuangalia kumbe walikuwa wamemjeruhi wamechoma kisu shingoni na kumbaka"

Kwa upande wa mama mzazi wa marehemu  amesema hakuwahi kulitegemea jambo hilo na kwamba limemuumiza kwani binti huyo anayemtaja kuwa ni mwanae wa kwanza alifanyiwa ukatili mkubwa sana.

Mwenyekiti wa mtaa wa Pasiansi Isaya Limbe amekiri kutokea kwa tukio hilo ambapo tukio hilo limetokea na kuahidi kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama katika kuwabaini wahusika wa tukio hilo
 

HABARI ZAIDI

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea

Bashiri Mohamed (35) Mwenye Koti Jeusi akiwa anafikishwa Mahakamani Ilemela, Jijini Mwanza

Aliyezini na binti yake apandishwa kizimbani