Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Rais Samia asisitiza elimu zaidi dhidi ya UKIMWI

Thursday , 1st Dec , 2022

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amesisitiza umuhimu wa kuzidisha elimu na kampeni kuhusu maambukizi ya UKIMWI kwani kumekuwa na ongezeko kubwa la maambukizi hasa kwa vijana wadogo

Rais Samia ametoa kauli hiyo mkoani Lindi katika maadhimisho ya siku ya UKIMWI duniani ambapo kitaifa yameadhimishwa mkoani humo

"Kuna maambukizi yanakuwa ya vijana wetu wa miaka 15 hadi 24, tusipozuia lile safari yetu itakuwa ndefu sana ya kutokomeza balaa hili, kwahiyo ni vyema tukaelekeza nguvu sana kwenye kampeni na elimu ya kusimamisha maambukizi"

Aidha Rais Samia amesisitiza umuhimu wa usawa ili kutokomeza ugonjwa huo ifikapo kwama 2030

"Kukosekana kwa usawa kunarudisha nyuma juhudi zetu za kutokomeza ugonjwa huu ifikapo mwaka 2030, hivyo ni muhimu tutumie maadhimisho haya tutafakari kwa kina na kuhakikisha tunaweka mikakati itakayoimarisha usawa"

Akizugumzia baadhi ya changamoto zilizopo mkoani Lindi ikiwemo suala la wanyama aina ya tembo kuvamia makazi ya watu Rais Samia amesema kumekuwa na changamoto kubwa inayotokana na wafugaji kuvamia katika maeneo ya wanyama hao 

"Wafugaji wameingia kwenye mapori yote, kwahiyo hata yale mapori ambayo tembo wamekuwa wakijificha yameingiliwa na wenyewe wametoka kuangalia makao mengine, lakini pia inawezekana jinsi tunavyotanua mashamba ya korosho na ufuta ndivyo tunavyosogea kwenye maeneo yao"

"Lindi huku kulikuwa hakuna ng'ombe, wamakonde wakiona ng'ombe walikuwa wanakimbia, sasa wafugaji wametoka walikotoka wamejaa tele Lindi, kwahiyo hata tembo waliopo Lindi hawakuwa wanajua ng'ombe hawajawahi kuwaona, kwahiyo wameona viumbe vigeni vimeingia na wenyewe wametoka, Wizara husika fanyeni kazi jambo hili" amesema Rais Samia
 

HABARI ZAIDI

Dkt. Selemani Jafo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

Hati miliki ardhi za kimila 4,450 kutolewa Mei 29

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao