Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mbegu za pamba zanusurika kuungua Shinyanga

Tuesday , 22nd Nov , 2022

Tani 210 za mbegu za pamba katika kiwanda cha Jielong kinachomilikiwa na raia wa china mjini Shinyanga kimenusurika kuteketea kwa moto baada ya ghala la kuhifadhia mbegu kuanza kuwaka moto upande wa mashudu na kuunguza sehemu kubwa ya ghala hilo

Katika tukio hilo wafanyakazi wanne waliokuwa wakifanya kazi ndani ya ghala hilo wamejeruhiwa na moto na kukimbizwa hospitali ya Rufaa Mkoa wa Shinyanga kwa ajili ya matibabu

Msemaji wa kiwanda cha Jielong Qir Fengzhou amesema moto huo ulianza kuwaka kidogo majira ya saa 11 jioni jana na wakaanza kuuzima lakini ghafula ulilipuka na kuwa mkubwa na kuomba msaada Jeshi la zimamoto na uokoaji Mkoa wa Shinyanga ambao walifika mapema kwa kushirikiana na magari mengine ya makampuni na kuanza kuzima moto huo kabla ya kusababisha madhara makubwa upande wa mbegu.

Mrakibu wa Jeshi la zimamoto na uokoaji Mkoa wa Shinyanga  Ramadhan Kano akiwa eneo la tukio,amesema wamefanya jitihada kubwa kuzima moto huo kutokana na kuwa mkubwa na kufanikiwa kuudhibiti kabla ya kusababisha madhara makubwa upande wa mbegu.

HABARI ZAIDI

Rose Senyagwa, Mchambuzi wa Masuala ya Hali ya Hewa kutoka TMA

Kimbunga "IALY" kinazidi kusogea Pwani ya bahari

Picha ya Diddy na Cassie enzi za mahusiano yake

Diddy aomba msamaha kumshambulia EX wake Cassie

Rais wa Iran Ebrahim Raisi

Rais wa Iran afariki kwa ajali ya Helikopta

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba,

China yaahidi kuendelea kufadhili miradi Tanzania

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu