Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Dkt. Biteko ataka maeneo ya madini yaendelezwe

Friday , 22nd Jul , 2022

Waziri wa Madini Dkt. Doto Biteko ametoa agizo kwa wawekezaji katika Sekta ya Madini kuendeleza maeneo yao yenye madini ya kimkakati badala ya kuyaacha bila kuyaendeleza suala linalopelekea wenye nia ya kuwekeza kukosa fursa hiyo

Amesema wapo wawekezaji wanaotaka kuwekeza katika Sekta hiyo maeneo mbalimbali nchini lakini wanashindwa sababu baadhi yao wanakaa na maeneo kwa muda mrefu bila kuyaendeleza.

Hayo yamebainishwa Julai 21, 2022 na Waziri wa Madini Dkt. Doto Biteko katika kijiji cha Mgambazi wilaya ya Uvinza Mkoani Kigoma alipotembelea Kampuni ya Lubalisi Resources Ltd inayofanya utafiti wa madini ya Nikeli.

Amewasisitiza wawekezaji katika Sekta ya Madini wanapaswa kufuata Sheria na Taratibu zilizowekwa katika uwekezaji huo ili kuepuka kufutiwa leseni zao.

Aidha, amewataka wawekezaji hao kuwasilisha taarifa za kipindi cha miezi mitatu ya utekelezaji kazi ya utafiti wa madini iliyofanyika kwa kipindi husika (quarterly report) ambayo husaidia kujua mwenendo au maendeleo ya mradi ya utafiti wa madini.

Amesema lengo la taarifa hizo ni kuiwezesha Serikali kutambua maendeleo ya mradi kwa kipindi husika.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Uvinza Hanafi Msabaha amewataka wawekezaji kuchangia katika huduma mbalimbali za kijamii ili jamii zinufaike na uwepo wa madini. Amesema ushirikishwaji wa wananchi utasaidia kupunguza malalamiko yanayojitokeza mara kwa mara kuhusu wawekezaji.

Naye, Mratibu wa Mradi na Mawasiliano ya Jamii Ashery Lemelo amemuakikishia Dkt. Biteko kusimamia maelekezo yaliyotolewa na Serikali katika mradi huo.

Katika wilaya ya Uvinza tafiti zinaonesha kuwa na madini ya Nikeli. Madini hayo hutumika katika utengenezaji wa bidhaa za magari ya umeme ikiwemo betri na vifaa mbalimbali vya umeme. Aidha, madini ya mkakati yenye uhitaji mkubwa nchini ni pamoja na madini ya Kinywe.
 

HABARI ZAIDI

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ

Muonekano wa Eneo la Somanga baada ya Mawasiliano kati ya Lindi na Dar es Salaam kurejeshwa.

Mawasiliano yarejeshwa barabara ya Dar - Lindi

Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga

Kituo cha kupoza umeme kujengwa Tunduma