Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Giggs ajiengua Wales kuelekea kombe la Dunia

Tuesday , 21st Jun , 2022

Aliyekua kocha mkuu wa timu ya taifa ya Wales Ryan Giggs ametangaza kujiuzulu rasmi nafasi ya kukinoa kikosi chataifa hilo, baada ya kusimama kazi hiyo tangu mwezi Novemba 2020 akikabiliwa na kesi ya unyanyasaji wa kijinsia alioufanya nyumbani kwake jijini Manchester.

Ryan Giggs aliyekua kocha wa Wales

Mchezaji huyo wa zamani wa Manchester United mwenye umri wa miaka 48 alishutumiwa kumshambulia na kumnyanyasa mpenzi wake wa zamani Kate Greville kati ya mwezi Agosti 2017 na Novemba 2020, lakini Giggs amekanusha tuhuma hizo na kukana mashitaka yote.

Katika taarifa yake, Giggs alisema: "Imekuwa ni heshima na nafasi ya pekee kuisimamia nchi yangu, lakini ni vyema shirkisho la soka la Wales, timu ya wakufunzi na wachezaji kujiandaa kwa ajili ya michuano ya kombe la dunia kwa uhakika, bila kuwaza kuhusu nafasi ya kocha mkuu."

Baada ya kutoa taarifa hiyo, Chama cha Soka cha Wales FAW kimetoa shukrani zake kwa Ryan Giggs kwa muda wake aliokuwa kocha wa timu ya taifa ya wanaume na inaheshimu uamuzi ambao amechukua, kwa manufaa ya soka ya la Wales.

Muda wote ambao Giggs alienguliwa kikosini timu ya Wales ilikua chini kocha msaidizi Robert Page aliyeiongoza Wales kufuzu michuano ya Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza baada ya miaka 64 bila Giggs. Page ndiye ataoingoza pia timu hiyo nchini Qatar baada ya Giggs kuamua kujiuzulu.

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea