Wednesday , 1st Jun , 2022

Kesi namba 77 ya Mwaka 2021 ilivyokuwa inawakabili wanachama 19 wa CHADEMA imeondolewa leo na Jamhuri kwa madai ya kutokuwa na nia ya kuendelea na kesi hiyo

Wanachama hao 19 wa CHADEMA walikamatwa tarehe 15.08.2021 wakiwa katika kanisa Katoliki la Kawekamo jijini Mwanza walipokwenda  kumuombea Mwenyekiti wa chama hicho  Freeman Mbowe alipokuwa anakabiliwa na  mashtaka ya ugaidi

Akizungumza nje ya Mahakama ya Hakimu mkazi Wilaya ya Ilemela Mwanza wakili wa wanachama hao Erick Mutta amesema kuwa shauri hilo limeondolewa kwa hati ya kufutiwa mashtaka iliyoletwa na Jamhuri na wao wamepokea uamuzi huo na sasa wanachama hao wapo huru

Mwenyekiti wa Baraza la Vijana Chadema BAVICHA John Pambalu ambaye ni moja ya viongozi wa Chadema waliohudhuria mahakamani hapo ameeleza kuwa Chama hicho kinaendelea kutoa wito kwa Jamhuri kufuta kesi za kisiasa ambazo zinawakabili wanachama na viongozi wa Chadema ili kufungua ukurasa mpya kisiasa nchini