Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mkiniona naharibu alaumiwe Makinda- Spika Ndugai

Friday , 11th Jun , 2021

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai amesema kuwa endapo ikitokea ameharibu katika kazi zake basi wa kulaumiwa ni Spika Mstaafu wa Bunge Mama Anne Makinda, kwani yeye ndiye aliyekuwa akimwongoza tangu awali.

Kushoto ni Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai, na kulia ni Spika wa Bunge Mstaafu Mama Anne Makinda

Kauli hiyo ameitoa Bungeni Dodoma, jana jioni Juni 10, 2021, wakati akimkaribisha Bungeni, na kuongeza kuwa Mama Makinda, amekuwa ni mwalimu wake kwa kipindi kirefu tangu alipoingia Bungeni kwa mara ya kwanza.

"Mama Makinda amekaa humu Bungeni takribani miaka 40 hii rekodi siyo rahisi na yeye alikuja kama mbunge kijana, nilipoingia hapa Bungeni nilipangwa kwenye Kamati ya Ardhi Maliasili na Mazingira na yeye akawa ni Mwenyekiti wangu, miaka mitano iliyofuata yeye akawa Mwenyekiti wa Bunge mimi akaniachia kijiti kwenye kamati," amesema Spika Ndugai.

"Baadaye akawa Naibu Spika mimi nikawa Mwenyekiti wa Bunge yeye akawa Spika wa Bunge mimi nikawa Naibu Spika, ameenda kustaafu nimekuwa Spika kwa hiyo mimi huwa nafuata mguu wake anapotoa mimi naweka sasa kwa vile alishastaafu na mimi nafuatia nitakuja kuwaambia huko mbele, namshukuru sana Mama kwa malezi mkiniona naharibu alaumiwe yeye maana yeye ndiyo mwalimu wangu kila hatua," ameongeza Spika Ndugai.

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya