Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Magufuli awapa siku 7 Waziri Gwajima na Jafo

Wednesday , 27th Jan , 2021

Rais Dkt John Magufuli, amewapa siku 7 Waziri wa Afya Dkt. Dorothy Gwajima na Waziri wa TAMISEMI Selemani Jafo, kuhakikisha wanaweka usawa katika suala la ugawaji wa madawa kwa mkoa wa Geita, kwani licha ya kwamba bajeti ya dawa imeongezeka lakini mkoa huo umekuwa ukipata dawa chache.

Kushoto ni Waziri wa Afya, Dkt. Dorothy Gwajima na kulia ni Waziri wa TAMISEMI Selemani Jafo.

Kauli hiyo ameitoa hii leo Januari 27, 2021, wakati akizindua majengo ya kituo cha afya cha Masumbwe, na ndipo alipobaini changamoto ya upunjwanji wa mgao wa madawa, licha ya kwamba bajeti ya madawa imeongezeka, hali aliyopelekea kutoa maagizo haya.

"Inawezekana kuna upunjaji wa mgawo wa madawa katika maeneo ya mkoa huu ikiwepo Masumbwe, bajeti ya madawa imeongezeka lakini dawa zinazotolewa katika mkoa huu ni chache, Waziri wa Afya na Waziri TAMISEMI mnaopanga bajeti ya madawa mkakae ndani ya siku 7 mje na majibu ni kwa namna gani madawa yataongezeka katika hospitali ya Masumbwe na maeneo mengine", amesema Rais Dkt. Magufuli.

Aidha Rais Magufuli pia aligusia suala la idadi ya watumishi wa afya katika Hospitali hiyo ya Masumbwe, na kuacha maagizo kwa Wizara ya Afya na TAMISEMI na kuzitaka ziwe na ushirikiano ili mambo yaende vizuri.
 

HABARI ZAIDI

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba