Rais wa Marekani Donald Trump.
Trump ametoa kauli hiyo kupitia ukurasa wake wa Twitter wakati ikiwa ni saa chache baada ya kushambuliwa kwa kambi hizo.
Trump ameandika kuwa "kila kitu kipo sawa, Kambi zetu mbili za Jeshi la Marekani zilizopo Iraq zimeshambuliwa na Iran, tunafanya tathmini kujua kama kuna waliopata madhara au uharibifu wowote wa mali, yote kwa yote tuna vifaa Bora vya kivita kuliko Nchi yoyote Duniani, nitatoa tamko hivi punde"
Kupitia Shirika la Habari la Uingereza BBC limeripoti juu ya kushambuliwa kwa kambi hizo mbili.
#KIMATAIFA Rais wa Marekani Donald Trump amesema nchi yake inafanya tathmini ya kambi zake mbili za kijeshi zilizopo Iraq ambazo zimeshambuliwa na Iran na anatarajia kutoa tamko muda sio mrefu. pic.twitter.com/R3rqp7habW
— East Africa Radio (@earadiofm) January 8, 2020

