Hayo yamebainishwa leo Disemba 30, 2019, na Evelina Magova na Grace Kivilo, ambao ni wazazi wa watoto waliokumbwa na mkasa huo, katika mkutano wa dharula ulioitishwa na Mkuu wa Wilaya hiyo Richard Kasesela, ambapo wamesema kuwa Mlay ana kituo cha kuchezesha michezo ya watoto 'Games' ambapo kwa nyakati tofauti alitumia nafasi hiyo, kuwafanyia ukatili watoto wao.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya hiyo Richard Kasesela, ameshtushwa na ukubwa wa tatizo hilo na kuchukua hatua ikiwa ni pamoja na kuunda kamati ya watu 10, ili kuendelea kubaini watoto ambao wamefanyiwa ukatili wakijinsia.
Mtuhumiwa wa ukatili huo kwa watoto mkoani humo, anaendelea kushikiliwa na jeshi la Polisi na upelelezi utakapokamilika atafikishwa mahakamani .

